NAIBU WAZIRI KAPINGA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MENEJIMENTI YA TPDC.

📌Awataka kuyapa kipaumbele masuala ya wafanyakazi.

📌Ataka changamoto ya wafanyakazi kukaimu muda mrefu kufanyiwa kazi.









MWANZA.

Naibu Waziri Nishati, Mhe. Judith Kapinga leo Septemba 17, 2024 amefungua kikao kazi cha Menejimenti ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Jijini Mwanza.


Lengo la kikao hicho ni kujitathmini, kujipanga na kukumbushana masuala mbalimbali ya Taasisi, ikiwemo maelekezo mbalimbali ya Serikali ya uendeshaji wa kampuni.


Amewasisitize na kuwakumbusha umuhimu wa kufanya kazi kwa umoja, ubunifu, weledi na upendo baina ya uongozi wa TPDC na wafanyakazi.


" Wizara ipo pamoja nanyi kuhakikisha azma na malengo makuu ya Serikali kwa TPDC yanafikiwa na zaidi", Amesisitiza Mhe. Kapinga. 


Aidha, amewakumbusha kuendelea kuyapa mkazo masuala yanayohusu wafanyakazi kwani ndio kiungo muhimu cha kufanikiwa kwa mipango na malengo mbalimbali ya TPDC.


"Ni vema masuala yanayohusu motisha zao ikiwemo mishahara kuhuishwa inapobidi na kuboreshwa kama hali ya kifedha inaruhusu", Amesema Mhe. Kapinga.


Ameongeza kuwa itasaidia kuwapa morali ya kuendelea kufanya kazi TPDC na kuvutia pia wafanyakazi wazuri sokoni.


Ametaka changamoto za wafanyakazi kukaimu nafasi za uongozi muda mrefu bila kuthibitishwa na changamoto za kupandishwa madaraja na nyinginezo zifanyiwe kazi ili kupunguza malalamiko kwa wafanyakazi.










Naibu Waziri Nishati, Mhe. Judith Kapinga leo Septemba 17, 2024 amefungua kikao kazi cha Menejimenti ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Jijini Mwanza.


Lengo la kikao hicho ni kufanya tathmini ya utendaji wa Menejimenti ya TPDC na kupanga mikakati mipya.

Hakuna maoni:

Inaendeshwa na Blogger.