DODOMA.
Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mha. Innocent Luoga amekutana na Naibu Balozi wa New Zealand nchini, Nicholas Meehan ambapo wamejadiliana kuhusu ushirikiano katika miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia rasilimali ya jotoardhi.
Kikao hicho kimefanyika leo, tarehe 4 Mei 2026, katika Ofisi za Wizara ya Nishati Mtumba jijini Dodoma.
Anesisitiza kuwa mradi wa AGF1 awamu ya kwanza umefika tamati lakini Tanzania inahitaji ushirikiano huo uendelee ili kuendeleza rasilimali ya jotoardhi ambapo Tanzania inalenga kuzalisha takribani MW 130 kutokana na nishati hiyoi ifikapo 2030.
Amefafanua kuwa, Wizara kupitia TGDC imepanga miradi miwili ya kimkakati itakayoweza kufanikisha lengo hilo ambayo ni mradi wa Ngozi utakaozalisha megawati 60 pamoja na Kiejo-Mbaka utakaozalisha megawati 70.
Aidha, ameiomba New Zealand kuangalia uwezekano wa kufadhili miradi hiyo ya kimkakati, pia kusaidia kutafuta ufadhili wa miradi hiyo.
Kikao hicho kimehudhuriwa na wataalam kutoka Wizara ya Nishati, TGDC, pamoja na wawakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.






Hakuna maoni: